ZILZALA NYENGINE YAZUKA IRAN
22 Februari 2005Matangazo
TEHERAN:
Kumetokea mtetemeko wa ardhi kusini-mashariki mwa Iran mapema hii leo ambamo watu si chini ya 190 wameuwawa na wengine 1000 wamejeruhiwa.Zilzala hiyo imetokea kandoni mwa mji wa ZARAND na katika mkoa wa KERMAN,km 700 kusini mashariki mwa mji mkuu Teheran.
Zilzala hii imefikia kipimo cha 6.4 cha RICHTER.