Zelensky: Putin anataka kuendeleza vita
29 Agosti 2025Akilihutubia taifa kwa njia ya video Alhamisi usiku, Zelensky amesema licha ya madai ya kuwa tayari kwa mazungumzo, malengo ya Urusi kuhusu vita hayajabadilika.
Maafisa wamesema mashambulizi hayo makubwa ya anga ya Urusi yalisababisha mauaji ya takribani watu 21 na kuwajeruhi wengine 48, na kuharibu ofisi za kidiplomasia za Umoja wa Ulaya.
Zelensky amesema mashambulizi hayo sio tu dhidi ya Ukraine, bali pia dhidi ya Ulaya na Rais wa Marekani, Donald Trump.
Ikulu ya Urusi, Kremlin imesema nchi hiyo bado ina nia ya kuendelea na mazungumzo ya amani, licha ya mashambulizi hayo yaliyotokea Alhamisi asubuhi.
Viongozi mbalimbali duniani wamekosoa vikali mashambulizi hayo, akiwemo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres na Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya, Kaja Kallas.