MigogoroUlaya
Zelensky: Kuna haja ya kubadili utawala nchini Urusi
31 Julai 2025Matangazo
Zelensky ametoa wito huo siku ya Alhamisi wakati akihutubia kwa njia ya mtandao mkutano wa Helsinki, unaoadhimisha miaka 50 tangu kusainiwa makubaliano ya kihistoria kati ya Marekani na Umoja wa Kisovieti yaliyosaidia kumaliza enzi za Vita Baridi.
Rais huyo wa Ukraine ameongeza kuwa kuna haja ya kubadili utawala nchini Urusi, akisema kuwa tofauti na hivyo rais Vladimir Putin ataendelea kuvuruga usalama wa majirani zake.
Zelensky ameyasema hayo wakati takriban watu sita wameuawa usiku wa kuamkia Alhamisi katika mji mkuu wa Ukraine-Kiev kufuatia mashambulizi yaUrusi.