Zelensky amtolea mwito Trump kuhakikisha mkutano na Putin
14 Mei 2025Zelensky hata hivyo amemtuhumu Putin kwamba hana nia ya dhati ya kuvimaliza vita kati ya Moscow na Kyiv.
Ameeleza kwamba mataifa ya Magharibi yanapaswa kuiwekea Urusi vikwazo zaidi iwapo Putin hatohudhuria mkutano huo, akisisitiza kwamba "atafanya kila awezalo” kuhakikisha mkutano huo unafanyika ili kufanikisha mpango wa kusitisha mapigano.
Soma pia: Merz: Urusi itawekewa vikwazo ikipuuza mchakato wa amani
Ikulu ya Kremlin imekataa kuweka wazi iwapo Putin atasafiri kwenda nchini Uturuki, baada ya kiongozi huyo mwenyewe kupendekeza kufanyika mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Urusi na Ukraine katika hotuba aliyoitoa mwishoni mwa wiki.
Mkutano wowote kati ya maafisa wa Urusi na Ukraine utakuwa wa kwanza wa ana kwa ana tangu miezi ya mwanzo ya uvamizi wa Urusi mnamo Februari mwaka 2022.