Zelensky akanusha kusaini makubaliano ya madini ya Marekani
22 Februari 2025Matangazo
Zelensky ameyasema hayo kufuatia kauli ya Rais wa Marekani Donald Trump anayeitaka Ukraine kuzipa kampuni za Marekani fursa ya uchimbaji madini, kama fidia ya makumi ya mabilioni ya dola za msaada uliotolewa chini ya utawala wa mtangulizi wake Joe Biden.
Marekani na Ukraine zazungumzia rasilimali asili za Kyiv
Siku ya Ijumaa, Mike Waltz, mshauri wa Trump wa masuala ya usalama wa taifa alidokeza kuwa Zelensky atatia saini mkataba huo hivi karibuni, lakini mkataba wa makubaliano hayo haukuwekwa wazi.