Zaidi ya watu 85 wauawa wakisubiri msaada Gaza
21 Julai 2025Matangazo
Vifo vingi vilitokea kaskazini mwa Gaza karibu na kivuko cha Zikim, ambako WFP ilisema malori 25 ya msaada yaliwasili lakini yakakumbwa na umati mkubwa.
Israel yatoa amri kwa wapalestina kuondoka katikati mwa Gaza
Afisa wa Umoja wa Mataifa alisema wanajeshi wa Israel walifyatua risasi kwa umati huo, huku video ikionyesha watu wakikimbia na milio ya risasi ikisikika.
Watu 26 wauawa Gaza kufuatia mashambulizi ya Israel
Wakati huo huo, jeshi la Israel lilitoa amri za uhamishaji kwa maeneo ya kati mwa Gaza, likiibua hofu mpya kwa mashirika ya misaada yaliyopo huko.