Zaidi ya watu 30 wauawa katika shambulizi la RSF, Sudan
22 Aprili 2025Matangazo
Kundi moja la wanaharakati linalofuatilia vita la Resistance Committees,
limesema kundi la RSF na washirika wake, lilifanya mashambulizi katika mji wa el-Fasher, mji mkuu wa jimbo la Darfur Kaskazini siku ya Jumapili ambapo mamia ya watu walijeruhiwa.
Jeshi la Sudan Kusini lauteka tena mji muhimu kutoka kwa wanamgambo
Wanaharakati hao wamesema kuwa RSF ilianzisha upya mashambulizi yake jana Jumatatu, na kuyashambulia kwa makombora majengo ya makazi na masoko ya wazi katika mji huo.
Hata hivyo, hakukuwa na tamko la mara moja kutoka kwa RSF.