JamiiAsia
Watu 150 hawajulikani walipo kufuatia mafuriko Pakistan
17 Agosti 2025Matangazo
Kwa mujibu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Maafa ya Mkoa wa Khyber Pakhtunkhwa, mafuriko hayo yamesababisha vifo vya watu wasiopungua 344 katika kipindi cha saa 48 zilizopita.Taarifa za sasa zinasema takriban waokoaji 2000, wanakabiliana na mvua na matope wakichimba nyumba zilizofunikwa na mawe makubwa katika jitihada za kukatisha tamaa za kuwatafuta walionusurika.Msemaji wa timu ya uokozi aliliambia shirika la habari la AFP kwamba "katika wilaya ya Buner ambayo imeathirika zaidi, watu 208 wamepoteza maisha na 'vijiji 10 hadi 12' vimefukiwa kwa maeneo fulani."