Watu zaidi ya 10 wauawa maandamano ya sabasaba Kenya
8 Julai 2025Matangazo
Wakati wa maandamano hayo ya Saba Saba, polisi walilazimika kutumia maji ya kuwasha kuwatawanya waandamanaji katika eneo la Kangemeni jijini Nairobi.
Mamlaka zililazimika kufunga barabara kubwa zinazoingia katika mji mkuu na shughuli nyingi za biashara zilifungwa kama njia ya kudhibiti machafuko.
Julai 7 yalipofanyika maandamano hayo ni siku ya kihistoria nchini Kenya inayojulikana kama 'Saba-Saba' inayoadhimisha sasa miaka 35 ya kuwakumbuka watu waliopigania demokrasia na mfumo wa vyama vingi mwaka 1990.