MigogoroMashariki ya Kati
Mashirika yatahadharisha kuhusu kuenea kwa njaa huko Gaza
23 Julai 2025Matangazo
Israel inakabiliwa na shinikizo kubwa la kimataifa kuhusu hali mbaya ya kibinadamu inayoendelea Gaza, ambako zaidi ya watu milioni mbili wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula na mahitaji muhimu kwa muda wa miezi 21 ya mgogoro.
Hata hivyo Israel imekuwa ikikanusha kuzuia msaada huo ikitangaza kuwa malori 950 tayari yapo Gaza na mashirika ya kimataifa yanasubiriwa kukusanya na kusambaza misaada hiyo kwa raia.
Marekani imemtuma mjumbe wake maalamu kwa Mashariki ya Kati, Steve Witkoff kuitembelea Ulaya wiki hii kujadili uwezekano wa kusitisha mapigano Gaza na kuhakikisha njia salama za utoaji misaada.