SiasaChina
Rais Xi Jinping alaani "tabia za uonevu"
1 Septemba 2025Matangazo
Xi amewatolea wito viongozi wa ushirika huo uliojikita kwenye masuala ya usalama kuheshimu usawa na haki na kuepuka fikra za Vita Baridi, ushindani wa makundi na tabia za uonevu.
"Kwanza, tunapaswa kuelewana, tukiweka kando tofauti. Matarajio ya pamoja ndiyo msingi wa nguvu yetu. Nchi wote wanachama wa SCO ni marafiki na washirika. Tunapaswa kuheshimu tofauti zetu, kuendeleza mawasiliano ya kimkakati, kujenga maelewano na kuimarisha mshikamano na ushirikiano."
Rais Xi aidha amesema katika hotuba yake ya ufunguzi ya mkutano huo unaoingia siku ya pili Jumatatu kwamba Beijing itashirikiana na pande zote za SCO ili kuimarisha usalama wa kikanda katika ngazi ya juu zaidi.