SiasaAsia
Gwaride kubwa la kijeshi lafanyika China
3 Septemba 2025Matangazo
Kando ya Xi, maadhimisho hayo yameshuhudiwa pia na Rais wa Urusi Vladimir Putin na mwenzake wa Korea Kaskazini Kim Jong Un. Katika sehemu ya hotuba yake mbele ya gwaride hilo Rais Xi alinukuliwa akisema, "lengo letu ni kukumbuka historia, kuwapa heshima mashujaa wetu, kuthamini amani na kuutengeneza mustakabali wetu. Historia imetufundisha kuwa imani katika haki haiwezi kuyumbishwa, matamanio ya amani hayawezi kuzuiwa na nguvu ya watu haiwezi kushindwa." Xi, amelikagua gwaride na silaha za kisasa zakivita huku helikopta za kijeshi zikiruka angani kwa dakika takriban 70 za maadhimisho hayo.