WHO: Kuna hatari ya kuenea kwa ugonjwa wa Chikungunya
23 Julai 2025Matangazo
WHO imesema imeshuhudia dalili zinazoshabihiana na zile zilizojitokeza mapema katika mripuko wa ugonjwa huo miongo miwili iliyopita na inajaribu kuzuia hali hiyo kujirudia.
Afisa wa WHO Diana Rojas Alvarez amesema Chikungunya ni ugonjwa usiojulikana sana, lakini umegunduliwa katika nchi 119 ulimwenguni, na hivyo kuwaweka watu bilioni 5.6 hatarini.
Chikungunya ni ugonjwa wa virusi unaoenezwa na mbu ambao husababisha homa na maumivu makali ya viungo na wakati mwingine unaweza hadi kusababisha kifo.